CCM Yarusha Jeshi La Anga Kuwakabili UKAWA Likiongozwa Na Mwigulu Nchemba.......Hapa Kuna Picha Wakipiga Push-Up Kumpa Sapoti Magufuli


Makada imara wa CCM  Field Marshall Mwigulu Nchemba na Dkt. Hamis Kigwangalla waki-Magufulika kuonesha sapoti kwa Mgombea wao Dkt. John Pombe Magufuli aliyefanya tukio hilo siku si nyingi kwenye Jukwaa la Kampeni.
Field Marshall Mwigulu Nchemba akilakiwa kwa nderemo mjini Nzega

Dkt Hamisi Kigwangalla akiwasili kwenye Ufunguzi wa kampeni za Ubunge jimbo la Nzega Mjini.Mjumbe wa timu ya Ushindi ya Chama cha Mapinduzi Field Marshall Mwigulu NChemba ambaye  ameanza safari za Anga-kwa-Anga kusaka kura Nchi nzima,Hapa akizungumza na Wananchi wa Nzega namna CCM ilivyosimamisha Mgombea Bora wa Urais ambaye sifa yake kuwa ni KAZI TU na rafiki yake Mkubwa ni TANZANIA. Comrade  Mwigulu amesema, Uchaguzi wa mwaka 2015 ni mwepesi sana kwa CCM  kwa kuwa wagombea wote ni zao la Chama tawala  na wanawajua vizuri. 

 Mbunge Ubunge wa jimbo la Nzega Mjini Ndg. Hussein Bashe akizungumza na Wananchi wake wakati wa Ufunguzi wa kampeni kwa Jimbo la Nzega Mjini. Bashe amewaomba Wana-Nzega kumpatia ridhaa ya kuwa mbunge wa Jimbo hilo ili aweze kusimamia vyema shughuli za Maendeleo kama Uimarishaji wa Huduma za Afya kwa Hospitali ya Nzega, Kusimamia haki za Bodaboda na Mamantilie wa Nzega, shughuli za Halmashauri ya Mji wa Nzega kwa Ufanisi.Pia amesisitiza yeye ni TEAM MAGUFULI na anaamini Maendeleo ya kweli na ya kasi yataletwa na Magufuli kwa awamu hii ya tano ya Uongozi wa Taifa letu.Mbunge Mtarajiwa wa Chama cha Mapinduzi Jimbo jipya la Nzega Vijijini Dkt. Hamis Kigwangala akisalimiana na Wananchi wa Nzega mjini alipokwenda kusapoti Ufunguzi wa kampeni za Mgombea Jirani Ndg.Hussein Bashe. Picha zote na Sanga Festo Jr

Share on Google Plus

    Blogger Comment