VITUKO KAMPENI ZA UBUNGE JIMBO LA IRINGA MJINI ,MGOMBEA NA MPAMBE WAKE WAZUNGUKA MITAANI NA BAISKELI KUHAMASISHA WATU KUFIKA KATIKA MKUTANO

 
Mgombea  ubunge  jimbo la Iringa mjini kupitia chama cha Democratic Party (DP)Bw Robarth Kisininiakizunguka mitaano kuhamasisha wananchi  kufika katika mkutano wake wa uzinduzi wa kampeni za ubunge pamoja na kunadi sera  za chama chake 




 
WAKATI  wagombea wa nafasi  za ubunge katika majimbo mbali mbali wa vyama vya  upinzani wakitumia nguvu kubwa ya kujinadi kwa kukodisha magari ya vipaza sauti  mgombea  ubunge jimbo la Iringa mjini kupitia chama cha Democratic Party (DP)Bw Robarth Kisinini amezindua kampeni zake za ubunge kwa aina ya  kipekee baada ya  kuzunguka mitaano na msafara wa Baiskeli mbili zenye vipasa sauti huku moja akiendesha mwenyewe akihamasisha watu  kufika katika mkutano wake .

Mgombea   huyo ambae  aliacha ngunzo la aina yake katika mitaa mbali mbali aliyopita  kuhamasisha  wananchi  kujitokeza  kwenye  uzinduzi  wa kameni zake  jana ,alisema amelazimika  kutumia usafiri huo  ili kuwaonyesha wananchi wa  jimbo la Iringa mjini  kuwa mbunge  wanaemtaka sio mbunge wa mbwembwe na matumizi ya nguvu  kubwa katika kampeni zake bali ni mbunge wa  kutumwa kama mwakilishi  wa wananchi bungeni.

Kwani  alisema  kuwa sababu hasa ya maendeleo ya  jimbo   hilo kwa miaka  mitano kutoonekana ni kutokana na aliyekuwa  mbunge wa  jimbo hilo mchungaji Peter Msigwa (chadema) kutumia muda  wake wa  miaka mitano kurudisha gharama  zake za kampeni badala ya  kuwaletea  wananchi wake maendeleo.

Hivyo alisema iwapo wagombea  ubunge wangefanya kampeni za gharama nafuu kama zake hali ya kimaendeleo katika  jimbo  hilo ingeweza  kuonekana ndani ya mwaka mmoja  pekee na  sio kuja na kauli ya  kuwa miaka mitano ya mbunge bila  kuleta maendeleo ilikuwa ni miaka ya  kujifunza kuwawakilisha  wananchi.

Bw Kisinini alisema nguvu kubwa  inayotumiwa na chama cha mapinduzi (CCM) kutaka kupokea jimbo hilo na nguvu  kubwa  inayotumiwa na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Mchungaji Msigwa kutaka  kuendelea  kuwa mbunge bila kufanya kazi ,ingeweza kutumika kuleta maendeleo katika jimbo hilo badala ya vyama  hivyo  kuvimbishiana misuli kwa kutumia gharama  kubwa ya kampeni.

" Jimbo la  Iringa mjini kwa miaka mitano limeshindwa kabisa kuwa na maendeleo kutokana na mvutano wa Chadema na CCM  hivyo  mimi  nimeamua kujitokeza ili  kuleta maendeleo ya  kweli katika miundo mbinu ,afya ,mazingira na kuona vijana  wanakuwa na maisha bora"

Kwani  alisema ubunge  wake  utakuwa tofauti na aliyekuwa mbunge wa  jimbo hilo mchungaji Msigwa kwani kwa upande wake kampeni  zake hazina gharama  kubwa  zaidi ya maji ya kunywa katika mikutano na chakula kwa kijana wake mmoja anaezunguka nae kuhamasisha  watu kufika katika mikutano yao ambayo hata 100,000 kwa muda  wote  uliobaki haitatumika.

Alisema wananchi  wa  jimbo hilo  watakuwa  wamefanya makosa iwapo  wataendelea  kutoa kura zao kwa  wale ambao walipata  kuwa  wabunge wa  jimbo hilo bila kuonyesha kazi  waliyoifanya na  kuwa njia pekee ya  kufanikiwa katika maendeleo ni kumchagua yeye (Kisinini)  kuwa mbunge wa maendeleo katika jimbo   hilo.

Kuhusu  vipaumbele  vyake  iwapo atakuwa  mbunge wa   jimbo  hilo alisema ni pamoja na  kuboresha huduma  za afya kwa  kuhakikisha  Hospitali ya wilaya  hiyo  iliyopo Frelimo inakuwa na madawa  na huduma  bora  zaidi ,pia  kuboresha  miundo mbinu katika mitaa mbali mbali na kuboresha sekta ya elimu 

MWISHO 
Share on Google Plus

    Blogger Comment